Home Habari za michezo ROBERTINHO MATATANI SIMBA, UONGOZI WATOA TAMKO HILI

ROBERTINHO MATATANI SIMBA, UONGOZI WATOA TAMKO HILI

Tetesi za Usajili Simba

Taarifa za ndani kutoka Simba zinaeleza kuwa Kibarua cha kocha wa Simba kipo mashakani hiyo ni baada ya Uongozi wa Simba kumpa mechi moja ya marudiano vs Power Dynamos endapo Simba itashindwa kufuzu basi watamfukuza.

Robertinho amepewa taarifa hiyo na uongozi huo baada ya sare ya ugenini waliyoipata Zambia na kuambiwa kuwa ili aendelee kusalia basi anatakiwa kuipeleka Simba kwenye makundi kwa kuwaondoa Power Dynamos.

Viongozi hawataki utani kabisa na Simba wamesajili vizuri wamempa Kila kitu kwahiyo wamempa mechi moja Simba lazima ifuzu hatua ya Makundi.

SOMA NA HII  BAADA YA KUFUNGWA MAGOLI YA 'KIZEMBE' JUZI....ALLY SALIM AIBUKA NA KUJITETEA KWA HILI...