Home Habari za michezo JE SIMBA WATAENDELEZA UBABE LEO!?

JE SIMBA WATAENDELEZA UBABE LEO!?

Habari za Simba

Wekundu wa msimbazi Simba SC, leo Oktoba 5, 2023 waashuka dimbani kukabilaiana na Tanzania Prisons ambapo swali la msingi ni; wataendeleza ubabe wa unbeaten ya 27?

Simba mpaka sasa, wanazo unbeaten 26 za Ligi Kuu ya NBC kutokea mwishoni mwa msimu uliopita ambapo kocha wao Roberto Oliviera ‘Robertinho’ ameendelea kushikilia bomba na kutopoteza mchezo hadi msimu wa 2023-24 ulipoanza.

Endapo ataibuka na ushindi hii leo, atakwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu kwani atakuwa na alama 12, nyuma yake atakuwa ni Azam FC mwenye alama 10 huku Yanga akiwa na alama tisa.

SOMA NA HII  SABABU ZA MAKOCHA MBAO FC KUBWAGA MANYANGA HII HAPA