Wakati mashabiki wa Simba baadhi wakiwa hawana imani na kipa Ayoub Lakred kutokana na kuruhusu mabao katika mechi mbili za kimataifa, tabasamu limeanza kuonekana baada ya Aishi Manula kuanza mazoezi ya uwanjani.
Manula ambaye ni kipa namba moja wa Simba, amerejea kwenye uwanja cha mazoezi mara baada ya kuwa nje muda mrefu akiuguza majeraha ya mguu.
Manula ameanza rasmi mazoezi na magolikipa wenzake ndani ya klabu hiyo tofauti na awali alipokuwa akifanya binafsi kwa takribani wiki tatu.
Kwa mujibu wa duru za habari kutoka kwenye uongozi wa Simba, zinasema kuwa Manula kwa sasa yupo tayari kwa ajili ya kukaa kwenye milingoti mitatu ya Simba.
Kocha wa Makipa wa Simba, Dani Cadena, alisema: “Haya ni mazoezi ya nne baada ya kuumia. Nina furaha kwa mabadiliko yanayoonekana kidogokidogo.”
Nauliza mchezaji wa yanga wa kimataifa Djuma Shabani kwa sasa yupo timu ipi akiitumikia msimu huu 2023/2024
Taarifa tulizonazo ni kuwa mchezaji huyo kasaini mkataba wa awali na Azam FC KWA AJILI YA MSIMU UJAO