HAJI MANARA AUMBUKA...NI BAADA YA KUMGOMBANISHA RAISI YANGA NA MTANGAZAJI
Habari za michezo

MANARA AKABIDHIWA KIPAZA SIKU YA MCHEZO WA MOROCCO

Staff Desk November 20, 2023 6:19 am

Kila mmoja wetu Mungu amemtunuku kitu special vile atakavyo. Wengi tuko tofauti katika vitu vingi, japo muda mwingine tunaweza kufanana katika hili na lile.

Jumanne tuna mechi ngumu kama nchi. Ni ngumu mno. Hii ni ngumu zaidi ya neno ngumu lenyewe. Kama Taifa tulipaswa kuitumia kila aina ya silaha tuliyonayo kumpiga adui Morocco.

Hapa ndiko anakoingia Haji Sunday Ramadhan Manara. Kinywa chake kinahitajika katika mechi hii. Haji ni moja ya silaha tulitonayo katika ghafla letu.

Haji ana ulimi wa kuujaza uwanja. Amewahi kufanya hivyo mara nyingi tu. Siandiki / sisemi haya kwa kuwa niko Manara TV na nimeamua kumsifia Boss wangu. Hapana! Jamaa anastahili.

Maana tunajuana. Baada ya mtu kuanza kuishambulia hoja iliyoko mezani mwake anaweza kuanza kumshamvulia mtoa hoja ambaye hamuoni na hayuko mezani mwake. TUNAJUANA.

Mechi ya Jumanne inakihitaji kinywa cha Haji kuhamasisha watu kuja kuujaza uwanja. Ushindi wa jana pale Morocco umerahisisha vitu vingi vya kuufanya uwanja ujae.

Mashabiki wetu wamezoea kuambiwa maneno fulani fulani hivi. Iandaliwe Press. Hapa Bongo Zozo na Manara, pale Hersi, Rais Karia na Try Again. Kisha yapigwe maneno na ikiwezekana kiingilio kiwe bure. Ikiwezekana lakini. Mechi hii tunataka alama tatu, hatutaki pesa.

Mechi za namna hii lazima tutumie watu tulionao kwenye masuala ya ushawishi katika mpira wetu ili kupata Full House pale kwa Mkapa.

Tanzania ni wamoja.

Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Taifa Stars.

HII SASA NDO INAITWA SIMBA NA MKATABA WA BALEKE……. NI UMAFIA TU RAIS SAMIA AIUNGA MKONO TAIFA STARS KWA STAILI HII

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply