Home Habari za michezo KAMA MASIHARA CHASAMBI AIKACHA YANGA……ATUA SIMBA STORY KAMILI IKO HIVI

KAMA MASIHARA CHASAMBI AIKACHA YANGA……ATUA SIMBA STORY KAMILI IKO HIVI

Tetesi za Usajili Simba SC

Nyota wa klabu ya Mtibwa Sugar Ladack Chasambi amesajiliwa na kikosi cha Simba kwa dau la million 70 na mshahara wa Million mbili [2] kila mwezi kwa miaka mitatu [3].

Chasambi imeitupilia mbali ofa ya Yanga ambayo ilikuwa na dau la usajili la Million 70 na mshahara wa Million sita [6] kwa mwezi, sababu kubwa ya kuitosa Yanga ni ufinyu wa nafasi ya kucheza kwenye kikosi hicho tofauti na Simba inayojitafuta.

Mbali na ofa Yanga ambayo aliipiga chini, ofa nyingine ilikuwa inatoka Azam FC mahali ambapo hakufikiria mara mbili kutokana na dau lao kuwa dogo, lakini pia klabu ya AS Vita ilikuwa inaihitaji saini yake.

Ladack ni miongoni mwa nyota wawili [2] ambao usajili wao umekamilika ndani ya klabu ya Simba kati ya sita [6] ambao wanatarajiwa kusajiliwa na klabu hiyo kwenye dirisha hili dogo la usajili la mwezi January.

Chasambi atakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kitakachoshiriki michuano ya mapinduzi yanayotarajiwa kuanza kurindima mwezi December.

SOMA NA HII  MGUNDA,ROBERTINHO WAIRARUA DYNAMO