Home Habari za Usajili NDOA YA DUBE NA AZAM IMEKWISHA…HUENDA AKATAMBULISHWA KESHO YANGA

NDOA YA DUBE NA AZAM IMEKWISHA…HUENDA AKATAMBULISHWA KESHO YANGA

Habari za Usajili, Prince Dube

Ni suala la muda tu, Prince Dube ‘Mwana wa Mfalme’ atatambulishwa kuwa mchezaji wa Yanga baada ya kuachana na Azam FC.

Azam FC walimkabidhi Dube ‘release letter’ baada ya kutimiza masharti aliyowekewa ambayo ni kurudisha fedha aliyokuwa amelipwa na Azam FC kwa ajili ya kuongeza mkataba

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF ndio iliyomaliza utata wa sakata la mkataba wa Prince Dube ambapo awali Azam Fc walikuwa wakidai ana mkataba na klabu hiyo mpaka mwaka 2026

Kamati ilibaini mkataba ambao Azam FC wanadai Dube alisaini ambao ungemfanya adumu katika klabu hiyo mpaka 2026, haukuwa umesajiliwa katika mfumo wa usajili FIFA Connect na hivyo PRINCE Dube kutakiwa arudishe fedha alizopewa na Azam Fc ili awe huru

Hicho ndicho kiilichotokea na sasa Dube ni mchezaji huru na anakwenda kujiunga na timu ya ndoto zake, Yanga

Safari ya Prince Dube kun’goka Azam Fc ilianza mwezi March 2024 pale alipotangaza kuachana na timu hiyo kwa kile alichoeleza hafurahishwi vile timu hiyo inaendeshwa

Kuondoka kwa Prince Dube katikati ya msimu hakutofautiani na tukio ambalo aliyekuwa kiungo wa Yanga Feisal Salum alifanya Disemba 2023

Unaweza kusema Wananchi wamejibu mapigo kwa kutumia njia ileile ambayo Azam Fc waliitumia kumn’goa Fei Toto Yanga

Wakati Fei Toto ametoroka Yanga, uongozi wa mabingwa hao wa nchi uliweka msimamo kwa kutaka taratibu zifuatwe ikiwa ni pamoja na kuitaka timu iliyokuwa ikimuhitaji Feisal ijitokeze lakini Azam Fc hawakufanya hivyo

Busara ikatumika kumruhusu Fei Toto kujiunga na Azam Fc baada ya ushauri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dk Samia Suluhu Hassan ambaye aliwataka viongozi wa Yanga kumaliza sakata la mchezaji huyo.

SOMA NA HII  MASKINI SHEVA HKO NDIPO ALIPO SASA