Home Habari za Simba Leo HAJI MANARA KUHUSU KUMSHAURI FEISAL KUCHEZEA SIMBA NA SIO YANGA

HAJI MANARA KUHUSU KUMSHAURI FEISAL KUCHEZEA SIMBA NA SIO YANGA

HABARI ZA YANGA-HAJI MANARA

Haji Manara ameoneshwa kuchukizwa na taarifa iliyokuwa inasambaa kwenye mitandao ya kijamii, ikimhusisha yeye kuzungumza na aliyewahi kuwa mchezaji wa Yanga na sasa ana kipiga na AZam FC, Feisal Salum Abdallah Fei Toto kwamba amemshauri akachezee Simba Sc na sio Yanga.

”Vingine vingi vya uongo tunaviacha, lakini hili sio la kuliacha na limefanywa kusudi kunigombanisha na Wanayanga,ni jambo la kimkakati na wanaolifanya soon watajipambanua hadharani!!

“ hawa Vijana wanatumika na kina nani kunichafua, Nawajua hata malengo yao ni nini?

“Sijaongea na Feisal kwa muda mrefu sana na siwezi kumshauri jambo hilo,,nna heshma kubwa Yanga na kwa mpira wa nchi hii, no matter kuna Wajinga wanataka kunifuta.

“Nilisafiri hadi Dubai kumshawishi Fei aendelee kucheza Yanga,ninawezaje leo nimshauri vinginevyo?

“Nipo nje ya football, Naombeni mniache na acheni kujaribu kufuta legacy yangu.

“Mnatunga Story haina source wala haina kichwa wala miguu.

“Vijana acheni kutumika na hao Mbuzi wanaowalipa visenti,hao wananiogopa na wanawatumia bila nyie kujijua

“Hivi mkishtakiwa mtajibu nini ? Mkiambiwa mlete ushahidi mnao?

“Hao Bata wanaowatuma mnadhani wataweza kuwasaidia lolote? Hapo wenyew mmefurahi kuwapost na mtascreenshot hii lakini irakuja kuwagharimu one day,, WWTCH IT

“Mnachafua Online tv zote kisa njaa njaa zenu, tunaonekana wote Wapumbavu, Watangazaji wa hovyo wasioweza kutofautisha R na L mnapataje uhalali wa kunijadili? waambieni wanaonichafua waje wenyewe kama kweli Wanaume kisawa sawa,ukimya wangu wa hivi sasa,usitafsirike ni unyonge,naepusha kikombe cha shari kisitukumbe.”Haji Manara!

SOMA NA HII  SIMBA KUACHANA NA KIPA WAO...SABABU NI HIZI

1 COMMENT

  1. […] kama tu Simba kule kwenye eneo la mbele wanashindana kukosa nafasi za kufunga, Ateba nafasi tatu zote kashindwa […]

Comments are closed.