TPL NDO ISHAISHA HIVYO, HIYO RATIBA YA FA INATISHA

0

BINGWA ndo kama alivyoshinda na Ligi Kuu Bara imemalizika huku timu nyingi zikiwa zimeambulia maumivu makubwa msimu huu.Ilikuwa ni aina moja ya ligi iliyokuwa na ushindani kwa timu chache ambazo zilikuwa zinashiriki ligi hali iliyopoteza ule mvuto na msisimko ambao ulianza awali.Kukosekana kwa mdhamini kumeziminya klabu nyingi na kufanya uendeshaji kuwa mikononi mwa viongozi wenyewe huku wachezaji wakitumia nguvu...

BEKI SIMBA ASAINI YANGA

0

Uongozi wa klabu ya Yanga umemalizana na beki Lamine Moro kwa kusaini mkataba wa miaka miwili.Moro ambaye ni raia wa Ghana, ambaye aliwahi kuja Simba kufanyiwa majaribio kipindi cha michuano ya SportPesa CUP, amefikia mwafaka kwa kusajiliwa na Yanga.Beki huyo sasa atakuwa Jangwani mpaka mwaka 2021 akiihudumia timu hiyo ambayo ni bingwa wa kihistoria katika Ligi Kuu Bara.Usajili huo...

YALIYOTOKEA MSIMU HUU YASIJIRUDIE KESHO, WACHEZAJI WAFUNDISHE ‘FAIR PLAY’ UWANJANI

0

LIGI Kuu Bara imeisha kiubishi kwa kuwa tumeshuhudia namna ilivyokuwa inakwenda kwa mwendo wa kuchechemea ila mwisho wa siku mshindi kapatikana.Simba anapaswa pongezi kwa kutetea ubingwa wake msimu huu kwani haikuwa rahisi kufikia malengo ambayo amejiwekea hivyo ni muda mwingine mzuri kwake kujipanga kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa msimu ujao.Msimu huu alifanya vizuri kwa kutinga hatua ya robo...

YANGA KUMALIZANA NA BEKI KISIKI WA KMC

0

IMEEELEZWA kwamba uongozi wa Yanga umeanza mazungumzo na beki wa kikosi cha KMC, Ally Ally 'Mwarabu' ili kupata saini yake msimu ujao.Mwarabu amekuwa kiongozi ndani ya KMC na kuifanya safu ya ulinzi kuwa kisiki kwani KMC imekuwa ni namba moja kwenye timu zilizotoa sare nyingi ikiwa imefanya hivyo mara 16 msimu huu.Habari zimeelezwa kuwa Yanga tayari wamefikia sehemu nzuri...

ALLIANCE FC KUIFUMUA SIMBA NA YANGA

0

UONGOZI wa Alliance FC ya mkoani Mwanza umesema kuwa msimu ujao lazima wawe moto hasa kwa kuwapata wachezaji wenye uzoefu watakoongeza nguvu kwenye kikosi chao.Alliance walianza kwa kusuasua msimu huu kabla ya kufanya maboresho kwenye kikosi chao kwa kuleta wachezaji wenye uzoefu pamoja na mabadiliko ya benchi la ufundi.Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Alliance, Jackson Mwafulango amesema...

MAURIZIO SARRI KUIBUKIA JUVENTUS

0

KOCHA Maurizio Sarri, ambaye ametwaa kombe la Europa League msimu huu akiwa na Chelsea, inasemekana ameshafikia muafaka na Juventus kwa ajili ya kuinoa timu hiyo kwa msimu ujao wa 2019/20.Juventus inataka kumchukua Sarri kutoka Chelsea ili kuchukua nafasi ya Massimiliano Allegri, ambaye anaondoka mwishoni mwa msimu huu.Sarri amebakiza miaka miwili katika mkataba wake wa kuinoa Chelsea, ambayo haijaweka wazi...

YANGA WAIPANGIA KIKOSI CHA MAUAJI AZAM FC

0

UONGOZI wa Azam FC, umesema kuwa wametumia mbinu moja kubwa ikiwa ni pamoja na mchezo wao dhidi ya Yanga kuandaa kikosi cha mauaji dhidi ya Lipuli.Mchezo wa mwisho wa Azam kwenye ligi walicheza na Yanga na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, hali iliyowapa kujiamini wachezaji kuelekea fainali ya FA.Azam itamenyana na Lipuli kwenye fainali ya kombe la FA...

OBREY CHIRWA ATAKA KUREJEA YANGA

0

IMEELEZWA Kuwa baada ya mshambuliaji wa Azam FC, Obrey Chirwa kuigomea klabu hiyo kuongeza mkataba mpya ndani ya klabu hiyo ameanza mazungumzo na kikosi cha Yanga ili kujiunga nao msimu ujao.Taarifa kutokana ndani ya Yanga zimeeleza kuwa Chirwa amekuwa akiwasiliana na viongozi wake wa zamani ili kuona namna gani anaweza kurejea tena kwenye kikosi chake cha zamani."Amekuwa akifanya mawasiliano...

Walcot asajiliwa Yanga.

0

Harakati za usajili wa Yanga zinaendelea kwa kasi kwa ajili ya kujiimarisha kwa ajili ya msimu ujao , baada ya kuteseka sana msimu huu.Imedhibitishwa rasmi kuwa Yanga imemsajili kiungo wa APR, Issa Birigimana ambaye huitwa Theo Walcot na mashabiki kutokana na aina ya uchezaji wake kufanana na Theo Walcot.Issa Birigimana amedhibitisha yeye mwenyewe kuwa msimu ujao atakuwa...

BAADA YA KUTWAA KOMBE, HAZARD KUSEPA CHELSEA

0

Eden Hazard, baada ya kutimiza jukumu lake ndani ya kikosi hicho kutwaa kombe la Europa League kwa kuifunga Arsenal mabao 4-1, amesema kuwa anataka kwenda Real Madrid. Hazard alifunga mabao 2 kati ya mabao 4-1 ambayo wameshinda mbele ya Arsenal na kutwaa kombe ikiwa ni mara ya kwanza kutwaa taji hilo mbele ya Meneja wao Maurizio Sarri.Baada ya mchezo kuisha, Hazard...