Uncategorized

RASMI HARUNA NIYONZIMA AACHANA NA SIMBA

admin June 28, 2019 12:18 pm

KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima, amewaaga mashabiki wa timu hiyo na kuwashukuru kwa yote waliyoshirikiana kwa kipindi cha misimu miwili ndani ya klabu hiyo.

Mkataba wa Niyonzima wa miaka miwili na Simba umemalizika hivi karibuni huku kukiwa hakuna dalili zozote za kuongezewa mkataba mpya na uongozi wa timu hiyo.

Ikumbukwe kuwa, kiungo huyo alijiunga na Simba msimu wa 2017/18 akitokea Yanga ambayo aliitumikia tangu msimu wa mwaka 2011 akitokea APR ya Rwanda.

Kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram, Niyonzima aliandika ujumbe mfupi wenye maneno ya kuwaaga mashabiki wa Simba.

Kiungo huyo mwenye udambwidambwi uwanjani, ujumbe wake ulisomeka hivi: “Nawashukuru kwa kumbukumbu tulizoweka pamoja, kadiri muda unavyokwenda ndiyo nitaweka wazi sehemu nitakayokwenda.”

Ikumbukwe Championi iliweka wazi mapema hatima ya mchezaji huyo ndani ya kikosi hicho kufuatia viongozi wa juu kunishikiza kutoongezewa mkataba mpya kutokana na madai ya kuwa msumbufu.

AJIBU PASUA KICHWA, AWAZIMIA SIMU MABOSI WA TP MAZEMBE AC MILAN YAFUNGIWA KUSHIRIKI MICHUANO YA ULAYA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply