Home Uncategorized NYOTA HAWA SABA WAPIGWA CHINI TIMU YA TAIFA YA TANZANIA

NYOTA HAWA SABA WAPIGWA CHINI TIMU YA TAIFA YA TANZANIA


TIMU ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inatarajiwa kuanza safari leo kuelekea nchini Misri ambako itaweka kambi kwa ajili ya michuano ya Afcon ambayo inatarajiwa kuanza Juni 21.


Wachezaji saba wameachwa na kocha wa kikosi hicho Emmanuel Ammunike na ataondka na nyota 32 kuiwakilisha nchi huku akieleza kuwa anawaacha nyota hao kutokana na uwezo wao wa kufanya mazoezi, nidhamu mbali na Kapombe ambaye hajawa fiti.

Wachezaji hao ni pamoja na Jonas Mkude (Simba), Ibrahim Ajib (Yanga), Ayoub Lyanga (Coastal Union), Ally Ally (KMC), Kassim Khamis (Kagera Sugar), Kennedy Wilson (Singida United) na Shomari Kapombe(Simba).

SOMA NA HII  MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA