Home Uncategorized KOCHA WA KMC ANASUBIRI MASAA TU KWA SASA KUTIMKIA AZAM FC

KOCHA WA KMC ANASUBIRI MASAA TU KWA SASA KUTIMKIA AZAM FC


IMEELEZWA kuwa tayari uongozi wa Azam FC umefikia hatua nzuri ya mazungumzo na kocha wa KMC, Etienne Ndayiragije kwa ajili ya kukinoa kikosi hicho hivyo anahesabiwa masaa tu kutambulishwa.

Ndayiragije ambaye alijiunga na KMC msimu wa mwaka 2018/19 kwa kandarasi ya mwaka mmoja akitokea Mbao imeelezwa amegomea kuongeza mkataba mpya ndani ya KMC.

Akiwa na KMC, ameweza kuonyesha ushindani na kufanya kikosi chake kutisha kwa kuwa ndani ya timu nne bora licha ya ugeni wake ndani ya ligi.

Habari za ndani zimeeleza kuwa mazungumzo ya awali na Azam FC yamekamilika na kilichobaki kwa sasa ni masaa tu ambayo ameambiwa atatambulishwa na uongozi wa Azam FC.

SOMA NA HII  KMC USOKWAUSO NA HARUNA NIYONZIMA WA SIMBA