Home Uncategorized IBRAHIM AJIBU ATOA LA MOYONI KWA YANGA

IBRAHIM AJIBU ATOA LA MOYONI KWA YANGA

BAADA ya kujiunga na Simba kwa kandarasi ya miaka miwili akitokea Yanga, aliyekuwa nahodha wa Yanga amewashukuru mashabiki na viongozi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika ujumbe huu:-

“Hakika ilikuwa miaka miwili bora sana kwangu, ndani na nje ya uwanja, Yanga ilikua sehemu ya familia yangu.

“Nitoe shukrani zangu za dhati kwa viongozi, benchi la ufundi, wachezaji na mashabiki kwa kuniamini na kuniunga mkono katika kila jambo.

“Ni mengi nimejifunza na nina amini yatanisaidia kunijenga zaidi kama wachezaji, asante sana, hadi wakati mwingine tena, wananchi, asante,” amesema Ajibu. 

SOMA NA HII  SIMBA YAZUNGUMZIA POINTI ZA YANGA