Home Uncategorized INTER MILAN NA MANCHESTER UNITED ZINAKOMOANA ISHU YA LUKAKU

INTER MILAN NA MANCHESTER UNITED ZINAKOMOANA ISHU YA LUKAKU


ROMELU Lukaku mshambuliaji wa Manchester United anatajwa kukamilisha dili lake la kujiunga na Inter Milan wiki ijayo huku United nao wakiwakomoa mabosi wa Milan.

Mabosi wa timu hiyo inayoshiriki Ligi ya Serie A wanahaha kuipata saini ya nyota huyo msimu ujao.

Milan imetenga dau la pauni milioni 54 licha ya kushindwa kufikia mchanganuo ambao mabosi wa United wanautaka kwa mshambuliaji huyo mwenye miaka 26.

United wanataka dau la pauni milioni 75 ambazo walilipa wakati wanamchukua nyota huyo Everton mwaka 2017.

SOMA NA HII  WAARABU WA MISRI WAPIDUA MEZA KIBABE MBELE YA SIMBA KWA NYOTA HUYU