Home Uncategorized KOCHA TANZANITE: TUNAKWENDA KUPEPERUSHA BENDERA YA TAIFA AFRIKA KUSINI

KOCHA TANZANITE: TUNAKWENDA KUPEPERUSHA BENDERA YA TAIFA AFRIKA KUSINI

BAKARI Shime, Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Wanawake chini ya miaka 20 ‘Tanzanite’ amesema kuwa wanakwenda kuperusha vema Bendera ya Taifa.

Tanzanite wanaondoka leo kuelekea nchini Afrika Kusini kwa ajili ya michuano ya COSOFA inayotarajiwa kuanza Agosti mosi mpaka 11 baada ya kualikwa na wameondoka na wachezaji 20 pamoa na viongozi wengine.

Shime amesema:-” Tumekuwa kambini kwa muda wa mwezi mzima hivyo tumewapata vijana 20 ambao wataiwakilisha nchi na kila mmoja ana jukumu lake la kufanya kwa ajili ya Taifa.

“Watanzania wawe na imani ya timu yao kwani tunakwenda kufanya kazi kwa ajili ya Taifa,” amesema.

SOMA NA HII  VITA YA TANZANIA PRISONS V AZAM FC LEO SI MCHEZO, REKODI ZAO NOMA