JUMA Kaseja, nahodha msaidizi wa timu ya Taifa ya Tanzania amesema kuwa nafasi ya kushinda kwa timu nchini Kenya ipo kikubwa ni sapoti kutoka kwa mashabiki.
Taifa Stars mchezo wa kwanza wa kufuzu michuano ya Chan inayotarajiwa kufanyika Cameroon 2020 ililazimisha suluhu ya bila kufungana dhidi ya Kenya uwanja wa Taifa mchezo wa marudio utakuwa Agosti 4 nchini Kenya.
Kaseja amesema : “Wao wameweza kupata sare kwenye ardhi ya nyumbani, basi nasi tunaweza kupata ushindi kwenye ardhi yao Kenya, makosa yetu benchi la ufundi litafanyia kazi nasi tunajipanga tukiaimini tuna nafasi ya kusonga mbele.
“Morali kwa wachezaji ni kubwa na kila mmoja anatambua kazi yake, kikubwa ni sapoti kwa mashabiki na dua,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.