Home Uncategorized NAMUNGO FC, MTIBWA SUGAR, MBAO FC ZAINGIA ANGA ZA MWADUI FC

NAMUNGO FC, MTIBWA SUGAR, MBAO FC ZAINGIA ANGA ZA MWADUI FC

MUSSA Mbissa mlinda mlango wa Mwadui FC amesema kuwa ana ofa ya timu tatu mkononi mwake zikitaka kupata saini yake.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mbissa amesema kuwa bado anafikiria ni timu ipi ataitumikia msimu ujao.

“Uwezo wangu umefanya timu nyingi zikubali na kunifuatilia pia, kwa sasa nina ofa tatu mkononi hivyo kwenye ofa kubwa ndipo nitasaini,” amesema.

Habari zinaeleza kuwa timu ambazo zinawinda saini yake ni pamoja na Mbao FC, Mtibwa Sugar, Namungo FC huku mabosi wake Mwadui FC pia wakiwa wanahitaji saini yake.

SOMA NA HII  KILICHOMLETA NINJA YANGA HIKI HAPA, KESHO NDANI YA CHAMPIONI JUMAMOSI