Home Uncategorized REAL MADRID YATAKA BALE ASEPE, ZINEDINE APEWA JUKUMU HILO

REAL MADRID YATAKA BALE ASEPE, ZINEDINE APEWA JUKUMU HILO


MENEJA wa Real Madrid, Zinedine Zidane amesema kuwa hana tatizo na mchezaji wake Gareth Bale ila klabu inahitaji asepe ndani ya kikosi hicho ifikapo kesho.

“Tunamatuamaini anaweza kuondola ndani ya kikosi muda si mrefu na itakuwa furaha kwa kila mmoja ndani ya timu tunafanya kazi suala la uhamisho wake kwenda timu nyingine sasa.

“Sina tatizo naye binafsi ila ni lazima hili litokee kwa kuwa kuna wakati mambo yanatokea na ni lazima yatokee tu hamna namna.

“Natakiwa kufanya maamuzi na tunatakiwa kufanya mabadiliko lazima yatokee hata mchezaji mwenyewe anajua inaweza kuwa ndani ya masaa 12 ama 48 labda anaweza kuibukia Spurs itakuwa vema kwa kila mmoja.” amesema. 

SOMA NA HII  PAMOJA NA UBINGWA..SIMBA SC KUCHUKUA TUZO ZOTE ZA LIGI KUU BARA