Home Uncategorized TANZANIA PRISON YATAJA SABABU YA KUANZA KAMBI MAPEMA

TANZANIA PRISON YATAJA SABABU YA KUANZA KAMBI MAPEMA

ADOLF Richard Kocha wa Mbeya City amesema kuwa tayari timu imeingia kambini kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao wa mwaka 2019-20 unaotarajiwa kuanza Agosti 23.

Richard amesema kuwa malengo ya kuingia kambi mapema ni kuandaa kikosi chenye ushindani msimu mpya.

“Msimu uliopita hatukuwa na matokeo chanya kwenye matokeo yetu hivyo tumeamua kuanza kambi mapema kuondoa yale makosa ya msimu uliopita.

“Msimu ujao utakuwa na ushindani nasi tupo tayari kuonyesha ushindani, hivyo kuingia kwetu kambini mapema kutatupatia muunganiko mzuri,” amesema.

SOMA NA HII  RUVU SHOOTING YAPIGA HESABU KALI MZUNGUKO WA PILI