Home Uncategorized YANGA YAZIDI KUWA YA MOTO, YAITWANGA MORO KIDS 2-0, BALINYA ATUPIA

YANGA YAZIDI KUWA YA MOTO, YAITWANGA MORO KIDS 2-0, BALINYA ATUPIA


Mabao ya Balinya na Paul Godfrey yameiwezesha Yanga kuibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Moro Kids leo mjini Morogoro.

Bao la Balinya limepatikana kwa njia ya penati

Yanga imefanikiwa kupata ushindi huo ukiwa ni mchezo wa kirafiki uliomalizika muda mchache uliopita.

Ushindi huo unakuwa wa pili mfululizo kwa Yanga baada ya mechi ya kwanza kushinda mabao 10-1 dhidi ya Tanzanite Academy.

Kikosi hicho kimeweka kambi mjini Morogor ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu mpya ujao kunako Ligi Kuu Bara.

SOMA NA HII  NDANDA, KAGERA SUGAR ZAIKOMALIA MWADUI FC