MWENYEKITI wa kundi la Mzizima Boxing Family Group (MBFG), Dr.Abdallah Mandai amewataka mashabiki wa mchezo wa boxing kujitokeza kwa wingi Agosti 30 ukumbi wa CCM Ilala Kata kushuhudia vipaji kwa vijana watakaopanda ulingoni.
Mashindano hayo ndiyo ambayo yaliweza kuwatengeneza mabondia maarufu Bongo kitaifa na kimataia kama Rashid Matumla, Francis Cheka na wengine wengi.
Akizungumza na Saleh Jembe, Mandai amesema kuwa lengo kubwa la kundi hilo ni kuinua vipaji kwa vijana wenye uwezo wa kupambana ulingoni.
“Tunajua kwamba kuna vijana wenye uwezo wa kupambana na hawapati nafasi hivyo ni fursa yao sasa kuonyesha namna gani wanaweza kupata nafasi.
“Agosti 30 ni siku nzuri kwa mashabiki wa boxing kujitokeza kuona namna ushindani wa vijana ulivyo, kuna vijana zaidi ya 100 ambao watapanda kwenye ulingo kwa utaratibu maalumu hivyo tunawaomba mashabiki wajitokeze,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.