Straika wa Yanga, Juma Balinya, juzi alimwagiwa noti za maana na mashabiki wa timu hiyo wanaoishi Bostwana.
Fedha hizo zilitokana na kufunga bao muhimu ambalo liliipa nafasi Yanga ya kuendelea kusalia kunako Ligi ya Mabingwa Afrika.
Balinya aliifungia Yanga bao mnamo dakika ya 42 katika mechi ambayo ilimalizika kwa ushindi wa 1-0 na kuiwezesha kukutana na Zesco United katika mchezo utakaofuata.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Yanga, Mshindo Msolla, amethibitisha ni kweli Balinya alipokea fedha hizo kutoka kwa mashabiki.
Aidha, Msolla, ameeleza kuwa wamepanga kuwapa fedha wachezaji wote waliokuwa kwenye msafara kama motisha na yote hii inachagizwa na ushindi wa juzi.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.