Home Uncategorized KMC WATAJA SABABU YA KUPOTEZA MBELE YA AS KIGALI LEO TAIFA

KMC WATAJA SABABU YA KUPOTEZA MBELE YA AS KIGALI LEO TAIFA

JUMA Kaseja nahodha wa timu ya KMC amesema kuwa kilichowaponza leo kushindwa kutusua mbele ya AS Kigali ni kuruhusu makosa yaliyowapa ushindi wapinzani wao AS Kigali.

Leo Uwanja wa Taifa, KMC ilikuwa inarusha kete yake ya pili kwenye michuano ya kimataifa dhidi ya AS Kigali mchezo wa marudio ambao umekamilika kwa KMC kupoteza kwa kufungwa mabao 2-1.

Bao la kwanza la AS Kigali lilifungwa dakika ya 29 kupitia kwa Rashid Kabisa dakika ya 63 Eric Nsabimana alimalizia bao la pili huku lile la kufutia machozi kwa KMC likifungwa na Yussuff Ndikumana dakika ya 87.

SOMA NA HII  UNAAMBIWA KELVIN YONDANI ANATISHA BALAA,KESHO NDANI YA SPOTIXTRA JUMAPILI