CRESCENTIUS Magori, Mtendaji Mkuu wa klabu ya Simba amesema kuwa maendeleo ya kikosi cha Simba kimataifa yapo sawa na wana matumaini ya kupata matokeo chanya.
Simba itamenyana na UD Songo mabingwa wa Msumbiji Agosti 6 wanatarajia kuondoka Ijumaa kwa ndege ya kukodi.
“Timu itaondoka Ijumaa asubuhi kuelekea Msumbiji kwa ndege ya kukodi na tutarejea baada ya mechi kumalizika kuja kujiandaa na mechi ya marudiano pamoja na ile ya ngao ya Jamii dhidi ya Azam.
“Tumefanya hivyo ili kukwepa usumbufu wa kuunganisha ndege mbili kwa wakati mmoja ilihali tunaweza kufanya mambo makubwa kwa ajili ya klabu yetu,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.