Home Uncategorized MBWANA SAMATTA AWAPA CHEMSHA BONGO MASHABIKI WAKE NAMNA HII

MBWANA SAMATTA AWAPA CHEMSHA BONGO MASHABIKI WAKE NAMNA HII


MBWANA Samatta, nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania leo ameacha swali kwa wadau mna mashabiki wake kwenye ukurasa wake wa Instagram akihitaji wamtabirie ni jibu gani amejibu.

Samatta ambaye kwa sasa anakipiga KRC Genk ya Ubelgiji ambao ni mabingwa watetezi ameandika namna hii: 

“Nilikuwa na mahojiano mazuri leo na radio GRK, nikijibu maswali ya mashabiki mtandaoni, kuna swali niliulizwa, kati ya KRC Genk kuchukua kombe la Champion League au Tanzania kucheza World Cup kipi utachagua, unadhani nilichagua kipi?

SOMA NA HII  HILI HAPA JESHI KAMILI LA WAZEE WA KUPAPASA RUVU SHOOTING DHIDI YA SIMBA