Home Uncategorized NAHODHA STARS AFICHUA SIRI YA MAFANIKIO

NAHODHA STARS AFICHUA SIRI YA MAFANIKIO


JUMA Kaseja, nahodha msaidizi wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ amesema kuwa siri kubwa ya ushindi ni kujiamini na kufanya kazi kwa kushirikiana.

Jana Stars ilishinda mchezo wake wa marudiano dhidi ya Kenya kwa penalti 5-1 kwenye mchezo wa kutafuta tiketi ya kufuzu michuano ya Chan inayotarajiwa kufanyika Cameroon 2020.

“Tunafanya kazi kwa ajili ya Taifa na kila mmoja anajua kwamba kikubwa ambacho mashabiki na watanzania wanakihitaji ni kupata ushindi kwenye michezo ambayo tunacheza hivyo ushindi wetu ni zawadi kwa watanzania na mashabiki wetu kiujumla,” amesema.

Hatua inayofuata kwa Stars ni mchezo dhidi ya Sudan kabla ya kufuz michuano ya Chan.

SOMA NA HII  POGBA AINGIA ANGA ZA PSG, WAMUUNGANISHA NA DI MARIA