Home Uncategorized NAHODHA YANGA AWAITA MASHABIKI KESHO TAIFA SIKU YA MWANANCHI

NAHODHA YANGA AWAITA MASHABIKI KESHO TAIFA SIKU YA MWANANCHI


PAPPY Tshishimbi, nahodha wa kikosi cha Yanga amewataka mashabiki kesho kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa kushushudia burudani.

Kesho ni kilele cha siku ya Mwananchi ambapo Yanga itatambulisha wachezaji wapya pamoja na jezi mpya.

Tshishimbi amesema:”Maandalizi yapo vizuri na kila kitu kipo sawa hivyo ni wakati wa mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanjani kuona timu yao ikipambana.

“Tumerejea salama na morali ni kubwa hii ni timu ya wananchi na kesho ni siku ya wananchi hivyo sapoti ni muhimu,” amesema.

Yanga kesho itacheza mchezo wa kirafiki na timu ya Kariobangi Sharks kutoka Kenya ambao ni mabingwa wa kombe la SportPesa.

SOMA NA HII  ASAINI MIAKA MITATU WILLIAN NDANI YA ARSENAL