JERRY Muro, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru mkoani ambaye aliwahi kuwa Ofisa Habari wa Yanga amewashangaa wanaodai kuwa Yanga ni timu dhaifu.
Muro amesema: “Nani anasema Yanga ni timu dhaifu? Yanga ni timu Bora msimu huu kuliko timu yoyote isipimwe uwezo wake kwa mechi za kirafiki itakuja kufanya balaa siku za usoni,” amesema.
Yanga ilipoteza hivi karibuni mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Polisi Tanzania uliochezwa Uwanja wa Ushirika Moshi Kwa kufungwa mabao 2-0 ambapo wafungaji walikuwa ni Marcel Kaheza na Ditram Nchimbi.
Mwinyi Zahera, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa sababu kubwa ya kushindwa kufurukuta mbele ya Polisi Tanzania ni ubovu wa Uwanja.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.