Home Uncategorized PIGO, SASA JUVENTUS KUSEPA NA NYOTA HAWA WATATU NDANI YA MANCHESTER UNITED

PIGO, SASA JUVENTUS KUSEPA NA NYOTA HAWA WATATU NDANI YA MANCHESTER UNITED


JUVENTUS imedaiwa kuhusishwa na mpango wa kusepa na wachezaji watatu ndani ya kikosi cha Manchester United ambao ni David de Gea, Eric Bailly na Nemanja Matic.

Licha ya kuwa tayari dirisha la usajili limefungwa lakini Juventus inaamini inaweza kufanya mipango ya kuwasajili wachezaji hao ambao inaonekana hawana furaha kwenye timu hiyo kwa sasa.

De Gea ni kipa namba moja ndani ya United licha ya makosa mengi ya hivi karibuni hajasaini mkataba mpya na hakuna dalili kama anaweza kusaini huku Bailly akiwa na majeraha makubwa ya muda mrefu na hana nafasi ndani ya United baada ya kutua Harry Maguire pia Matic amecheza mara moja tu mbele ya Scott McTominay.

SOMA NA HII  VIDEO: KOCHA WA SIMBA AZUNGUMZIA KUHUSU MIPANGO YAKE, KESHO KUANZA MAZOEZI