Home Uncategorized SASA MBABE AANZA KUMWAGA TAMBO, MCHINA AMPA KIBURI

SASA MBABE AANZA KUMWAGA TAMBO, MCHINA AMPA KIBURI


ABDALAH Panzi ‘Dulla Mbabe’ bingwa wa  ubingwa wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Duniani (WBO) Asia Pacific uzito wa kati (Super Middle) ambao aliupata hivi karibuni kwa kumtwanga Zulipikaer Maimaitiali raia wa China amesema kuwa kwa sasa atamchapa kila anayekuja mbele yake.

Ushindi huo ambao umempa heshima Mbabe ulimpa fursa ya kupeleka mkanda huo bungeni aliupata kwa kumnyoosha mpinzani wake kwa TKO raundi ya tatu umeipandisha chati Tanzania kwa upande wa ngumi.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mbabe amesema kuwa ana imani na kile ambacho anakifanya kutokana na maandalizi ambayo anayafanya jambo linalompa matumaini kuwafundisha adabu mabondia watakaohitaji kupambana naye.

 “Mchina amenijengea uwezo wa kujiamini na kunifanya nione kwamba ninaweza kupambana na yoyote atakayetaka pambano nami hivyo sitakuwa na huruma nitamchapa kila ajaye kwangu,” amesema.

SOMA NA HII  ARSENAL YACHANA MKEKA, YAPIGWA NA ASTON VILLA