Home Uncategorized SASA NYOTA MMOJA WA STARS NI MILIONEA AOGA MINOTI YA KUTOSHA

SASA NYOTA MMOJA WA STARS NI MILIONEA AOGA MINOTI YA KUTOSHA


KUTOKANA na kazi aliyofanya jana uwanja wa Taifa kwa kuokoa penalti moja na kuwapotezea uwezo wa kujiamini na akukosa penalti mbili sasa Juma Kaseja anaongelea minoti ya kutosha.

Stars jana iliibuka kidedea mbele ya Burundi kwenye mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu Kombe la Dunia kwa ushindi wa penalti 3-0 baada ya dakika 90 120 kukamilika kwa kufungana bao 1-1.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ameandika namna hii kwenye ukurasa wake wa Instagram:”Kwa kweli Mungu anazidi kutuonyesha upendo wake Hongera watanzania hongera Taifa.

” Kama tulivyoongea usiku pale Hyatt hotel wachezaji wote mmetimiza kiapo chenu nami nawaomba kwa muda wenu nitimize kiapo changu kwenu.

” Mwisho kila mchezo una nyota naomba nimpatie Milioni 10 ndugu yetu Juma Kaseja kama nyota wangu,”. 

SOMA NA HII  AZAM FC WATAJA HOFU YAO ILIPO NDANI YA LIGI KUU BARA