Home Uncategorized KINACHOIBEBA COASTAL UNION CHATAJWA

KINACHOIBEBA COASTAL UNION CHATAJWA



KOCHA Mkuu wa Coastal Union, Juma Mgunda amesema kuwa kinachoibeba timu yake kupata matokeo chanya ni kujituma kwa wachezaji wake na kufuata kile ambacho wanaelekezwa.


Akizungumza na Saleh Jembe, Mgunda amesema kuwa ugumu wa ligi unawafanya wachezaji wake wajitume na kupambana kutafuta matokeo.

“Wachezaji wangu napenda kuwapa pongezi kwani wanafanya kazi ambayo inawapa furaha wao na mashabiki ni kitu kizuri.

“Kikubwa ni kwamba wanatambua kile ambacho mashabiki wanahitaji na wao wanafanya kile ambacho ninawaelekeza ni jambo la kuwapongeza,” amesema.


Coastal Union ipo nafasi ya pili kwenye msimamo ikiwa imecheza jumla ya mechi 17 ipmejikusanyia jumla ya pointi 30 kibindoni,
SOMA NA HII  NYOTA YANGA MTAMBO WA MABAO AOMBA KUSEPA