Home Uncategorized KIUNGO BORA WA SIMBA SASA KUTUA YANGA

KIUNGO BORA WA SIMBA SASA KUTUA YANGA


INAELEZWA kuwa Kiungo bora kwa msimu wa mwaka 2018/19 alipokuwa Simba, James Kotei yupo kwenye mazungumzo na Uongozi wa Yanga ili ajiunge na mabingwa hao wa kihistoria waliotwaa ubingwa mara 27.

Habari zinaeleza kuwa, Kotei ambaye alisepa Simba msimu wa 2018/19 baada ya kandarasi yake kumeguka na kujiunga na Kaizer Chiefs kwa sasa yupo kwenye hesabu za Yanga ili aongeze nguvu ndani ya kikosi hicho ambacho kimeanza kurejea kwenye kasi yake.

“Kotei yupo kwenye hesabu za kutua Yanga kwa sasa kutokana na uwezo wake mkubwa ambao anao, dirisha dogo wanajipanga kuongeza nguvu ukizingatia kuwa kocha mpya ameletwa,” alieleza mtoa taarifa huyo.

SOMA NA HII  VPL: MTIBWA 0-0 SIMBA