Mtibwa Sugar 0-0 Simba
Kipindi cha kwanza
Uwanja wa Jamhuri, Morogoro
MTIBWA Sugar leo wameikaribisha Simba Uwanja wa Jamhuri, Morogoro ukiwa ni mchezo wa mzunguko wa pili.
Simba iliyo chini ya Sven Vandenbroeck inapambana leo ikiwa na maumivu ya kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 na JKT Tanzania sawa na Mtibwa Sugar iliyopoteza kwa kufungwa bao 1-0 na Lipuli.
Mashabiki waliojitokeza ni wengi kushuhudia mchezo wa leo ambao ni wa kisasi kwa timu zote mbili.