Home Uncategorized HAJJI APEWA MIKOBA YA KUINUSURU MBAO KUSHUKA DARAJA

HAJJI APEWA MIKOBA YA KUINUSURU MBAO KUSHUKA DARAJA


ABDULMUTIK Hajji amepewa mikoba ya kuwa Kocha Mkuu wa timu ya Mbao FC ya Mwanza.

Awali Hajji alikuwa Kocha Msaidizi ndani ya kikosi hicho na bosi wake alikuwa ni Hemedd Morroco ambao wote kwa pamoja waliamua kusepa kutokana na mwenendo mbovu wa timu pamoja na madai ya kutolipwa stahiki zao.

Mbao kwa sasa ipo nafasi ya 18 ikiwa na pointi 22 imecheza mechi 23 imeshinda mechi tano kazi yake kubwa itakuwa kuinusuru timu hiyo kushuka daraja kutokana na nafasi iliyopo kwa sasa.
SOMA NA HII  SIMBA SASA WAGEUZIA HASIRA ZAO TPL, WAPANIA KUIMALIZA MAPEMA MTIBWA SUGAR