UONGOZI wa Simba umesema kuwa umejipanga kufanya kweli kwenye mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa uwanja wa Uhuru, Septemba 17.
Akizungumza na Saleh Jembe, Meneja wa Simba, Patrick Rweyemamu amesema kuwa kikosi kipo sawa na kinaendelea na maandalizi kwa ajili ya mchezo huo.
“Hatuna jambo lingine la kufanya kwa sasa kwenye michuano ya kimataifa sasa nguvu zetu tunaziwekeza kwenye ligi.
“Mchezo wetu unaofuata ni dhidi ya Mtibwa Sugar kazi ni kubwa kutafuta matokeo chanya na nina imani tutafanya vema.” amesema.
Simba msimu huu imekwama kusonga mbele kama msimu uliopita ambapo ilitinga hatua ya robo fainali baada ya kutolewa na bao la ugenini na timu ya UD do Songo imekwama kusonga mbele.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.