Home Uncategorized SIMBA SASA WAGEUZIA HASIRA ZAO TPL, WAPANIA KUIMALIZA MAPEMA MTIBWA SUGAR

SIMBA SASA WAGEUZIA HASIRA ZAO TPL, WAPANIA KUIMALIZA MAPEMA MTIBWA SUGAR


UONGOZI wa Simba umesema kuwa umejipanga kufanya kweli kwenye mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa uwanja wa Uhuru, Septemba 17.

Akizungumza na Saleh Jembe, Meneja wa Simba, Patrick Rweyemamu amesema kuwa kikosi kipo sawa na kinaendelea na maandalizi kwa ajili ya mchezo huo.

“Hatuna jambo lingine la kufanya kwa sasa kwenye michuano ya kimataifa sasa nguvu zetu tunaziwekeza kwenye ligi.

“Mchezo wetu unaofuata ni dhidi ya Mtibwa Sugar kazi ni kubwa kutafuta matokeo chanya na nina imani tutafanya vema.” amesema.

Simba msimu huu imekwama kusonga mbele kama msimu uliopita ambapo ilitinga hatua ya robo fainali baada ya kutolewa na bao la ugenini na timu ya UD do Songo imekwama kusonga mbele.

SOMA NA HII  HIKI HAPA KINACHOMBEBA PAUL NONGA WA LIPULI