Home Uncategorized KOCHA AMPELEKA HAALAD APELEKWA REAL MADRID

KOCHA AMPELEKA HAALAD APELEKWA REAL MADRID


ERLING Haaland yupo tayari kujiunga na Real Madrid. Hiyo ni kwa mujibu wa kocha wa zamani wa Byrne FK, Alf Ingve Berntsen ambaye alimnoa straika huyo miaka ya nyuma.
Haaland alikuwa chini ya Berntsen tangu akiwa na miaka nane hadi 15. Kwa sasa straika huyo ana miaka 19 ambapo alianza kung’ara na Red Bull Salzburg kabla ya Januari, mwaka huu kuhamia Borussia Dortmund.
“Kama ningekuwa kocha wa moja kati ya klabu tano kubwa duniani, ningemsajili.

“Nadhani yupo tayari kuichezea Real Madrid na huko atafanikiwa sana.”

Erling ana miaka 19 tu na anaendelea kuonyesha ubora wake, kama klabu kubwa zitashindwa kumsajili kwa sasa zitajutia huko mbele,” alisema kocha huyo.
SOMA NA HII  SENZO - TULIENI..MAMBO MAZURI YANAKUJA MSIMBAZI