Home Uncategorized JKT TANZANIA: TUPO TAYARI KUVAANA NA AZAM FC, SAPOTI YA MASHABIKI

JKT TANZANIA: TUPO TAYARI KUVAANA NA AZAM FC, SAPOTI YA MASHABIKI


ABDALAH Mohamed,’Bares’, Kocha Mkuu wa JKT Tanzania amesema kuwa leo vijana wake watapambana mbele ya Azam FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Uwanja wa Jamhuri.

Azam FC imeshatia timu mkoani Dodoma, leo itakuwa na kazi ya kumenyana na JKT Tanzania mchezo wake wa tatu ikiwa ugenini.

Bares amesema:”Kikosi kipo tayari na kila mchezaji amepewa majukumu yake ya kufanya, sapoti ya mashabiki inahitajika,”.

Azam FC ilitoka kumalizana na Ndanda na Namungo, nyanda za juu kusini na iliambulia pointi moja na kupoteza nne kati ya sita baada ya kupata sare moja na Ndanda kisha ikachapwa na Namungo FC bao 1-0.

SOMA NA HII  LAMPARD, CHELSEA KIMEELEWEKA