Home Uncategorized NEYMAR KUIKOSA NANTES LEO

NEYMAR KUIKOSA NANTES LEO

PARIS Saint-Germain (PSG) itamkosa mshambuliaji wake raia wa Brazil, Neymar Jr kwenye mchezo wa Ligue 1 utakaochezwa leo dhidi ya Nantes kutokana na majeruhi.

Neymar alicheza dakika 90 kwenye mchezo wao uliopita dhidi ya Montpellier ambao walikubali kichapo cha mabao 5-0.


Kwa sasa PSG ipo nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa Ligue 1 ikiwa imecheza jumla ya mechi 22 ina pointi 55.

Mpinzani wake Nantes ipo nafasi ya tisa ikiwa na pointi 32 imecheza pia mechi 22.

SOMA NA HII  RAIS MAGUFULI AUMIZWA NA KUONDOKA KWA MUGABE, ATOA TAMKO