Home Uncategorized SIMBA KUIFUATA LIPULI YA IRINGA LEO

SIMBA KUIFUATA LIPULI YA IRINGA LEO


BAADA ya kikosi cha Simba kupata ushindi wa mabao 3-0 mbele ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri Morogoro, leo kinaifuata Lipuli, Iringa.

Simba ambao ni vinara wa ligi wakiwa na pointi 53 watakaribishwa na Lipuli Februari 15, Uwanja wa Samora.

Mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Uhuru, Simba ilishinda kwa mabao 4-0 jambo litakalofanya mchezo uwe wa kisasi kwa Lipuli.

Lipuli ipo nafasi ya 9 ikiwa na pointi zake 29 kibindoni zote zimecheza mechi 21.

SOMA NA HII  KARIAKOO DABI,SIMBA QUEENS V YANGA PRINCESS VITA YA KUTIBUA REKODI