Home Uncategorized YANGA YAINYOOSHA GWAMBINA KWA BAO MOJA LA KIDEO, YATINGA HATUA YA ROBO...

YANGA YAINYOOSHA GWAMBINA KWA BAO MOJA LA KIDEO, YATINGA HATUA YA ROBO FAINALI


YANGA leo imetinga hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Gwambina FC mchezo uliochezwa Uwanja wa Uhuru.

Bao pekee la ushindi kwa Yanga lilifungwa na kiungo mshambuliaji Haruna Niyonzima dakika ya 45 kwa shuti kali alilofunga akiwa nje ya18.

Ushindi huo unaifanya Yanga isonge hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho lililo mikononi mwa Azam FC ikisubiri droo ipangwe kujua mpinzani wake.


Gwambina FC ilipambana kipindi cha pili kurudisha bao hilo uimara wa mlinda mlango Metacha Mnata na umakini wa beki kisiki Lamine Moro ulitibua mipango yao.
SOMA NA HII  KOCHA MAMELODI AMCHANA MAYELE KISA VISA