Home Uncategorized DILI LA DRINKWATER NDANI YA ASTON VILLA MIKONONI MWA MABOSI

DILI LA DRINKWATER NDANI YA ASTON VILLA MIKONONI MWA MABOSI


DANNY Drinkwater ambaye alijiunga kwa mkopo ndani ya Klabu ya Aston Villa kwa sasa anasubiri hatma yake kujua kama ataendelea kubaki ndani ya kikosi hicho ama la.
Nyota huyo alijiunga kwa mkopo mwezi Januari akitokea klabu ya Chelsea aliyokuwa akiitumikia ili kujiweka fiti.
Inaripotiwa kuwa mwenye sauti ya mwisho juu ya hatma ya kiungo huyo ni bosi wa Aston Villa ambaye mpaka sasa hajasema jambo lolote.
Nyota huyo inaelezwa kuwa aliingia kwenye mgogoro na baadhi ya wachezaji wenzanke ikiwa ni pamoja na Jota kwenye mazoezi walipokuwa ndani ya Uwanja wao wa Villa Park jambo ambalo limepelekea uongozi wa klabu kudaiwa kuwa watamtoza faini nyota huyo mwenye miaka 30.
SOMA NA HII  ISHU YA MWAMNYETO KUIBUKIA YANGA, MSIMAMO WA COASTAL UNION UPO HIVI