Home Uncategorized YANGA YAGAWANA POINTI MOJAMOJA NA AZAM FC, MABAO MAWILI YA AZAM YAMEYEYUKA...

YANGA YAGAWANA POINTI MOJAMOJA NA AZAM FC, MABAO MAWILI YA AZAM YAMEYEYUKA MAZIMA

YANGA imegawana pointi moja leo mbele ya Azam FC kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Taifa.

Kasi ya Azam ilianza kipindi cha kwanza ambapo walifunga bao la kwanza kupitia kwa Abdalah Kheri mwamuzi alisema kuwa tayari mfungaji ameotea.

Licha ya timu zote kupambana kwa hali na mali kusaka pointi tatu hakuna aliyepata bao kipindi cha kwanza ambapo timu zote zilikwenda mapumziko ubao ukisoma 0-0.

Tabia ya kujidondosha mara kwa mara kwa mchezaji David Molinga kulimponza kwani alichezewa faulo ndani ya 18 na mchezaji wa Azam FC ngoma ikapeta ikaendelea kama hakuna jambo lililotokea.

Kwa upande wa Azam pia, Nocolas Wadada alichezewa naye faulo ndani ya 18 , mwamuzi hakuamua iwe penalti maisha yakaendelea kusaka pointi tatu.

Dakika ya 48, Wadada alifunga bao kwa upande wa Azam FC lilikataliwa kwa kile mwamuzi alichoeleza kuwa ameotea.

Mbali na Luc Eymael kufanya mabadiliko kipindi cha pili kwa kumtoa Patrick Sibaomana nafasi yake ikachukuliwa na Morrison , Ditram Nchimbi nafasi yake kuchukuliwa na Makame, Molinga nafasi yake kuchukuliwa na Yikpe Gnamien bado mambo yalikuwa magumu.

Kwa Azam FC, Andrew Simchimba aliingia akichukua nafasi ya Richard Djod alionekana kubadilisha mchezo ila bado mambo yalikuwa ni magumu kwa timu zote mbili.

Sare hiyo inaifanya Azam FC kukusanya poi nti nne mbele ya Yanga ambpo kwenye mchezo wa kwanza, Azam ilishinda bao 1-0 na leo sare inawafanya wasepe na pointi moja.

SOMA NA HII  MANARA: CORONA IMETIBUA DILI LA WAZUNGU KUJA BONGO