YANGA wakati inalazimisha sare ya kufungana bao 1-1 ilikosa huduma ya wachezaji wake sita wa kikosi cha kwanza huku taarifa zikieleza kuwa wamegoma ndani ya klabu hiyo.
Uongozi wa Yanga umesema kuwa hakuna suala hilo ila kuna sababu maalumu ambazo zimewakumba wachezaji wao.
Wachezaji hao ambao walikosekana kwenye mchezo wa jana uliopigwa Machi 15 Uwanja wa Majaliwa ni pamoja na Haruna Niyonzima, Kelvin Yondani, Lamine Moro, Mohamed Issa ‘Mo Banka’, Adeyum Saleh na David Molinga.
Sababu za nyota hao kuukosa mchezo wa jana zipo namna hii:- Haruna Niyonzima alikuwa na kadi tatu za njano.
Kelvin Yondani alipewa ruhusa ya Mwalimu kwasababu za kifamilia,David Molinga ambaye yeye aliomba ruhusa kutokana na Mkewe kuwa mgonjwa.
Lamine Moro, Mohamed Issa (Mo Banka) na Adeyum Saleh.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.