Home Uncategorized MEDDIE KAGERE KUMBE KWA PENALTI HAJAMBO,CHEKI MABAO ALIYOFUNGA NA ALIYOKOSA

MEDDIE KAGERE KUMBE KWA PENALTI HAJAMBO,CHEKI MABAO ALIYOFUNGA NA ALIYOKOSA

MEDDIE Kagere mshambuliaji wa Simba ndani ya kikosi cha Simba amepewa jukumu la kupiga penalti.

Kwenye jumla ya mabao 19 ambayo Kagere amefunga kwenye Ligi Kuu Bara, mabao manne amefunga kwa mipira iliyokufa kutokana na kuwa mpiga penalti mkuu.

 Simba ikiwa imepiga jumla ya penalti sita yeye amepiga tano amekosa moja huku moja ikifungwa na Hassan Dilunga mbele ya Lipuli FC Uwanja wa Uhuru.

 Amefunga mbele ya Yanga, Kagera Sugar mara mbili na Mbeya City huku akikosa penalti moja mbele ya Biashara United zote alipiga kwa guu lake la kulia.

SOMA NA HII  MSHAMBULIAJI WA YANGA APANIA KUFANYA MAKUBWA, KIWANGO CHAKE ADAI HAKIJAMFURAHISHA