Home Uncategorized MEDDIE KAGERE: NINAIPENDA KAZI YANGU

MEDDIE KAGERE: NINAIPENDA KAZI YANGU


MEDDIE Kagere, mshambuliaji wa Simba amesema kuwa anapenda kazi yake ya mpira jambo linalomfanya afurahie kufunga kila wakati akiwa ndani ya uwanja.

Ligi Kuu Bara kwa sasa imesimama ili kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona wakati ligi ikisimama, Kagere alikuwa amefunga mabao 19.

Kagere amesema:”Ninaipenda kazi yangu ndio maana nikiwa ndani ya uwanja ninafunga na ninafurahi pamoja na wachezaji wenzangu.

“Ninatambua kuwa kazi kubwa ya mchezaji ni kutimiza majukumu yake kwa wakati,” .

SOMA NA HII  UNAAMBIWA AJIB NI ZAIDI YA AZIZ KI