LIONEL Messi nahodha wa Barcelona, amesema kuwa jambo la wachezaji kukatwa mshahara limechelewa kufanyika kwa sababu wachezaji walikuwa wanapambana kuisadia klabu pamoja na kuwasiaidia wale walioathirika.
Hatua hiyo ya kukatwa mshahara huo ni kwa ajili ya kuwachangia wafanyakazi wa Barcelona kulipwa mshahara pamoja nakuwasaidia waathirika wa Virusi vya Corona.
Uongozi wa Barcelona umekubaliana kuwakata wachezaji asilimia 70 ya mishahara.
Messi,amesema:- “Kwetu wakati umefika, tutakatwa asilimia 70 ya mishahara yetu katika kipindi hiki. Pia tutaisaidia klabu ili wafanyakazi wengine walipwe asilimia 100 ya mishahara yao nadhani suala hili lilichelewa,” .
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.