JOSE Mourinho, Kocha Mkuu wa Spurs amesema kuwa kwa sasa kwake mambo ndani ya kikosi hicho ni magumu kutokana na aina ya kikosi alichonacho.
Mourinho alipigwa chini jumla kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kufungwa mabao 3-0 mbele ya RB Leipzing na kufungashiwa virago kwa jumla ya mabao 4-0 hatua ya 16 bora.
“Tatizo nililonalo kwa sasa ni ugumu wa kikosi changu nilichonacho sio rahisi kunipa matokeo mazuri na hili sioni likiisha kesho kwa kweli niwe muwazi mambo bado magumu,” amesema.
Spurs itakuwa na kibarua kingine Jumapili mbele ya Manchester United kwenye mchezo wa Ligi Kuu England.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.