Home Uncategorized NONGA: UBORA WA WACHEZAJI WENZANGU UNANIFANYA NAKUWA BORA

NONGA: UBORA WA WACHEZAJI WENZANGU UNANIFANYA NAKUWA BORA

PAUL Nonga, nahodha wa Lipuli amesema kuwa kinachomfanya kuwa bora ndani ya Lipuli ni kutokana na ubora wa wachezaji anaocheza nao.

Nonga ni miongoni mwa manahodha wazawa wenye mabao mengi ndani ya Ligi Kuu Bara akiwa amefunga mabao 11 nahodha mwingine mwenye mabao sawa na Nonga ni Reliants Lusajo anayekipiga Namungo.

Akizungumza na Saleh Jembe, Nonga amesema kuwa kinachombeba ndani ya Lipuli ni pamoja na ubora wa wachezaji ambao anacheza nao kwa kuelewana na kupeana majukumu.

“Aina ya wachezaji ambao ninacheza nao pamoja na namna ambavyo kila mmoja anapokea majukumu aliyopewa ni vitu muhimu kuzingatia kwani vinaongeza ubora,” amesema.

SOMA NA HII  AZAM FC WABABE WA WACONGO KAZINI LEO FAINALI