UONGOZI wa Yanga umesema kuwa utaonyesha soka safi lisilo na makandokando kwenye mchezo wao utakaochezwa Machi 8, Uwanja wa Taifa dhidi ya Simba.
Yanga iliyo chini ya Luc Eymael itakutana na Simba kwenye mchezo wa pili wa Ligi Kuu Bara ikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare ya kufungana mabao 2-2 Januari 4.
Ofisa Uhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz amesema:” Mashabiki wa Yanga ni siku yetu kuonyesha soka lisilo na makandokando na kila mchezaji anajua jukumu lake tupo tayari kuonyesha soka safi kwa kuwa tumejipanga na tunaamini inawekezakana.
“Kwenye mchezo wetu dhidi ya Simba tuna kazi moja ya kutafuta ushindi ukizingatia kwamba tumetoka kumalizana na Mbao na kupata ushindi mnono wa mabao 2-0,”.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.