Home Uncategorized ALIYEZITESA SIMBA NA YANGA KWA SASA ANAPATA TABU KWELI

ALIYEZITESA SIMBA NA YANGA KWA SASA ANAPATA TABU KWELI

KASSIM Khamis, kiungo anayekipiga Azam FC anapitia wakati mgumu kwa sasa ndani ya klabu yake mpya hiyo.

Simba na Yanga zilikuwa kwenye mvutano mkubwa wa kuinasa saini ya jamaa huyu wa Zanzibar ila mabosi wa Azam FC wakawazidi ujanja na kuipata saini ya nyota huyu aliyekuwa akikipiga Kagera Sugar.
Amepita mikono ya makocha wawili alianza na Etienne Ndayiragije ambaye kwa sasa yupo na timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kisha sasa Azam ipo chini ya Arstica Cioaba ila hana nafasi kikosi cha kwanza.
Alitupia mabao saba akiwa Kagera Sugar msimu wa 2018/19 alipata nafasi ya kuitwa kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania lakini kwa sasa anaishi dunia nyingine hafurukuti kikosi cha kwanza anaishia kusugua benchi.

SOMA NA HII  ISHU YA YAKUB MOHAMED KUIBUKIA SIMBA IMEFIKIA HAPA